Tuesday, 12 September 2017

Korea Kaskazini: Tutailetea Marekani machungu makubwa

Korea Kaskazini: Tutailetea Marekani machungu makubwa

Haki miliki ya picha Getty Images
Image caption Korea Kaskazini inasema imeunda na kulifanyia majaribio bomu la haidrojeni
Korea Kaskazini imetishia Marekani na kusema kuwa itasababisaha machungu makali ambayo Marekani haijawai kushuhudia kufuatia vikwazo vipya vilivyowekwa na Umoja wa Mataifa.
Mjumbe wa Korea Kaskazini katika Umoja wa Mataifa ameishutumu Marekani kwa kutafuta makabiliano ya kisiasa , kiuchumi na kijeshi.
Mapema Marekani iliapa kuweka shinikizo zaidi ikiwa Korea Kaskazini itaendela na njia zake hatari.
Haki miliki ya picha Getty Images
Image caption Korea Kaskazini imekuwa ikifanyia majaribio makombora yake
Vikwazo vya Umoja wa Mataifa ni hatua ya kuhakikisha kuwepo uhaba wa mafuta na kipato kufuatia mipango yake ya nyulia.
Hatua hizo zinapiga marufuku uuzaji mafuta kwenda Korea Kaskazini na uuzuaji wa bidha kutoka Korea Kaskazini baada ya jaribio la sita na kubwa zaidi la bomu la nyuklia mapema mwezi huu.
Han Tae Song, ambaye ni balozi wa Korea Kaskazini kwenye Umoja wa Mataifa alisema amekataa kile alichokitaja kuwa vikwazo vilivyo kinyume na sheria.
"Hatua zitazochukuliwa na Korea Kaskazini zitaisababishia Marekani machungu makali ambayo hajawai kushuhudiwa katika historia yake," aliambia mkutano huko Geneva.
Haki miliki ya picha Getty Images
Image caption Umoja wa Mataifa umeiwekea vikwazo mara kwa 

No comments:

Post a Comment

Watoto bado wanafanya kazi migodini, shambani’

Watoto bado wanafanya kazi migodini, shambani’   0 By Elizabeth Edward, Mwananchi eedward@mwananchi.co.tz Da...