Friday, 13 October 2017

Watoto bado wanafanya kazi migodini, shambani’

Watoto bado wanafanya kazi migodini, shambani’









By Elizabeth Edward, Mwananchi eedward@mwananchi.co.tz
Dar es Salaam. Licha ya Serikali na wadau mbalimbali kupigia kelele suala la ajira kwa watoto, wengi wameendelea kufanya kazi kwenye migodi na mashamba.
Utafiti uliofanywa na Kigoda cha Taaluma cha Mwalimu Nyerere umebaini kuwa watoto hufanya kazi katika maeneo hayo huku umaskini ukitajwa kuwa chanzo.
Utafiti huo ulifanyika katika migodi ya Mirerani, Buhemba na Uvinza na kwenye mashamba ya tumbaku (Urambo), mpunga (Mvomero) na nyanya (Ilula).
Akiwasilisha matokeo ya utafiti huo, mtafiti Dk Novetha Kigombe alisema watoto wengi waliohojiwa wameeleza kuwa wanafanya kazi hizo ili wapate kipato kwa ajili ya familia zao.
Pia, alisema wazazi wamekuwa wakiwatuma ili washiriki kuongeza kipato cha familia kwa lengo la kukabiliana na umaskini.
“Katika kazi hizo watoto wanakutana na athari mbalimbali, kwanza wanaathirika kisaikolojia. Pia wengi wanaacha masomo ili wapate muda mwingi wa kufanya kazi,” alisema Dk Kigombe.
Katika kukabiliana na hali hiyo mwanasheria kutoka Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Joyce Komanya alisema ipo haja ya suala hilo kuwekewa sheria kali zaidi.
Alisema kama kungekuwapo na hatua kali za kisheria zinazochukuliwa dhidi ya kampuni au mwekezaji anayeajiri watoto tatizo hilo lingepungua.
Mwenyekiti wa Kigoda cha Taaluma cha Mwalimu Nyerere, Profesa Penina Mlama alisema kufanyika kwa utafiti huo ni sehemu ya kumuenzi Mwalimu Julius Nyerere.     

IGP SIMON NYAKORO SIRRO AFUNGUKA KUHUSU MAGE KIMANGE

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Nyakoro Sirro amefunguka na kusema kuwa jeshi la polisi linatambua makosa ya kimtandao yanayofanywa na mwanadada Mange Kimambi na kusema kuwa jeshi la polisi linashughulikia suala hilo.

IGP Sirro amesema hayo jana  alipokuwa mjini Iringa kwenye ziara ambapo alisema kuwa jeshi la polisi linatambua uvunjifu wa sheria ya makosa ya kimtandao yanayofanywa na mwadada huyo maarufu mitandaoni ambaye amekuwa mkosoaji wa mambo mbalimbali na kutoa machapisho ambayo serikali inaona ni ya matusi na kashfa kwa serikali na viongozi wake.

Aidha IGP Sirro alisema kuwa kwa sasa hawawezi kuweka wazi ni hatua gani zinachukuliwa dhidi ya mwanadada huyo ambaye kwa sasa anaishi nchini Marekani

Mbali na hilo  IGP Sirro alisema jeshi hilo halitawavumilia maafisa wa polisi na askari wanaowasaidia watu wanaofanya unyanyasaji kwa watoto kwa kuwafanyia vitendo vya ubakaji na ulawiti ili kukwepa mkono wa sheria huku akiwataka wananchi wanaohisi kutotendewa haki katika kushughulikia makosa ya aina hiyo kupeleke malalamiko kwa wakuu wa mikoa na viongozi wengine.



Thursday, 12 October 2017

MAREKANI YAJIONDOA UNESCO IKILALAMIKIA UBAGUZI DHIDI YA ISRAEL

Marekani yajiondoa Unesco ikilalamikia ubaguzi dhidi ya Israel


Haki miliki ya pichaAFP
Image captionMarekani yajiondoa Unesco ikilalamikia ubaguzi dhidi ya Israel
Marekani inajiondoa kutoka shirika la elimu sayansi na utamaduni la Umoja wa Mataifa UNESCO ikililaumu kwa ubaguzi dhidi ya Israel.
Wizara ya mambo ya kigeni ilisema kuwa itabuni ujumbe wa waangalizi kwenye shirika hilo lenye makao yake nchini Ufaransa kuchukua mahala pa uwakilishi wake.
Mkuu wa Unesco Irina Bokova, alisema kujiondia kwa Marekani ni hatua ya kujutia.
"Kujiondoa kwa Marekani ni pigo kwa familia ya Umoja wa Mataifa," Bi Bokova alisema.
Mwaka 2011 Marekani ilifuta bajeti yake kwa Unesco kupinga hatua yake ya kuwapa wapalestina uanachama kamili.
Rais wa Marekani Donld Trump awali amekosoa kile alichotaja kuwa ni mchango mkubwa wa Marekani kwa mashirika ya Umoja wa Mataifa.
Marekani hutoa asilimia 22 ya bajeti ya kawaida ya Umoja wa Mataifa na asilimia 28 kwa shughuli za amani za Umoja wa Mataifa.
Unesco iko katika mikakati ya kumteua kiongozi mpya huku mawaziri wa zamani wa Qatari na Ufaransa, Hamad bin Abdulaziz al-Kawari na Audrey Azoulay wakiwa sako kwa bako kuchukua mahala pa Bokova.

Thursday, 5 October 2017

‘Tume ilivyotimiza sheria uteuzi wabunge wa Cuf

0 Comments
TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) hivi karibuni ilifanya uteuzi wa Wabunge Wanawake wa Viti Maalumu kwa tiketi ya Chama cha Wananchi (CUF), uteuzi uliopokelewa kwa hisia tofauti na baadhi ya wadau.
Baadhi ya wafuasi wa CUF, viongozi wa chama hicho na gazeti moja la Kiswahili ni miongoni mwa wadau walioshambulia Tume kwa madai kwamba kulikuwa na njama kati ya Tume na Spika wa Bunge, katika kulishughulikia suala la wabunge wanawake wa CUF waliofukuzwa uanachama na kusababisha uteuzi wa wabunge wengine kujaza nafasi zao.
Suala hili liliibua mjadala miongoni mwa wanajamii na Tume ikalaziamika kutoa ufafanuzi kwa ajili ya kuielimisha jamii ili kuziba mwanya wa ufahamu ambao umesababishwa na upotoshaji pamoja na ukosefu wa uelewa juu ya namna ambavyo Tume inafanya kazi zake.
“Nadhani tatizo hapa ni ukosefu wa uelewa wa watu kwa upande mmoja, lakini kwa upande mwingine kuna upotoshaji wa makusudi kabisa, pia inaonekana kuna watu hawajui na hawataki kujua,” anasema Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC, Kailima Ramadhani.
Anasema NEC imezingatia matakwa yote ya kisheria yanayohusiana na viti maalumu vya wabunge wanawake kwa kuzingatia kwamba sheria zinazoiongoza Tume zinatambua chaguzi za aina mbili, ule wa kupiga kura na ule wa wabunge wa kuteuliwa.
“Ifahamike kwamba viti maalumu vya wanawake ni aina ya uchaguzi kwa mujibu wa sheria, wabunge wanapatikana kwa njia mbili, ile ya kupiga kura na hii ya viti maalumu ambayo inatokana na uwiano wa kura kwa kila chama,” anasema.
Kailima anasema kwa bahati mbaya baadhi ya wapotoshaji ni viongozi wa CUF ambao kwa nafasi zao wanajua vizuri kanuni na taratibu ambazo zilifuatwa na tume kwenye mchakato huo. “Labda nianze kwa kuelezea viti maalumu vya wanawake vinatoka wapi?
Kwa mujibu wa Katiba Ibara ya 78 (1) na taratibu zilizowekwa, vyama vya siasa ambavyo vimeshiriki uchaguzi mkuu na kupata angalau asilimia tano ya kura za wabunge vinakuwa na sifa ya kupata wabunge wa viti maalumu vya wanawake ambavyo ni asilimia 40 ya wabunge wote,” anafafanua Kailima.
Ibara ya 78 (1) ya Katiba inasema “Kwa madhumuni ya uchaguzi wa wabunge wanawake waliotajwa katika ibara ya 66 (1)(b), vyama vya siasa vilivyoshiriki katika uchaguzi mkuu kwa kufuata utaratibu uliowekwa, na kupata angalau asilimia tano ya kura zote halali za wabunge, vitapendekeza kwa Tume ya Uchaguzi majina ya wanawake kwa kuzingatia uwiano wa kura ambazo kila chama kimepata katika uchaguzi wa wabunge”.
Kifungu namba 86A cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi kinavipa vyama vya siasa nafasi ya kuwasilisha kwa tume ya uchaguzi majina yanayopendekezwa kuteuliwa kwenye viti maalumu vya wanawake. “Chama cha siasa kinachogombea katika uchaguzi wa ubunge utakaofanyika baada ya kuvunjwa kwa Bunge kinaweza kupendekeza kwa tume majina ya wagombea wanawake wenye sifa kwa uteuzi wa viti maalumu kwa wanawake,” kinasomeka Kifungu 86A (1) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi.
Kailima anasema ili kutimiza matakwa ya kisheria, wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 Tume iliviandikia vyama vya siasa kuwaomba watume orodha ya majina wanayopendekeza kwa ajili ya viti maalumu vya wanawake bungeni.
Anasema kwenye mchakato wa kujaza nafasi za wabunge wanawake wa viti maalumu, Tume imekuwa ikivigawa viti kwa vyama ambavyo vimefanikiwa kupata asilimia tano ya kura za wabunge na katika uchaguzi wa mwaka 2015 vyama vilivyofanikiwa kuwa na sifa ni pamoja na Chama cha Mapinduzi (CCM), Chama cha Wananchi (CUF) na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
Kifungu namba 37 (3) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi kinasema: “Endapo mbunge anajiuzulu, kufariki au anaachia ofi si yake kwa sababu nyingine tofauti na zile zilizopo chini ya kifungu cha 133 (kuhusu kesi inayosubiria maamuzi ya mahakama), Spika, kwa maandishi kwa mwenyekiti wa tume na kwa taarifa itakayochapishwa katika gazeti la serikali, atatangaza kwamba kuna nafasi katika kiti cha ubunge”.
Kailima anazidi kufafanua kwamba baada ya NEC kupokea barua kutoka kwa Spika, hatua inayofuata inatekelezwa kwa mujibu wa Ibara ya 74 (4) ya Katiba ambayo inaelekeza kwamba orodha iliyowasilishwa tume awali na chama husika cha siasa wakati wa uchaguzi mkuu itumike kujaza nafasi iliyopo wazi au nafasi zilizo wazi. Anasema ujazaji huo wa nafasi unafanyika baada ya kushauriana na chama husika cha siasa.
“Orodha ya majina ya wagombea wanawake iliyowasilishwa kwa Tume ya Uchaguzi na kila chama kwa ajili ya uchaguzi mkuu ndiyo itakayotumiwa na Tume ya Uchaguzi baada ya kushauriana na chama kinachohusika, kwa madhumuni ya kujaza nafasi yoyote na mbunge wa aina hii inapotokea wakati wowote katika maisha ya bunge,” inasomeka Ibara ya 78 (4) ya Katiba.
Kailima anasema kutokana na matakwa ya sheria kwa kawaida tume inaviandikia vyama vya siasa barua kuwauliza ni yupi miongoni mwa wale walioko kwenye orodha anafaa kuteuliwa kujaza nafasi iliyoachwa wazi.
Anasema vyama hivyo vinatakiwa kujibu barua ya Tume kwa kujaza Fomu Namba 8E, na baada ya kuipokea hiyo fomu Tume huendelea na taratibu nyingine za kiutawala kujiridhisha kwamba mhusika au wahusika wana sifa stahiki na kupitisha jina au majina yao.
Anasema vigezo vya kuwa na sifa vinatokana na matakwa yaliyowekwa na sheria kuhusu sifa za mtu anayefaa kuwa mbunge lakini ni lazima kwanza jina linalopendekezwa liwe kwenye orodha iliyowasilishwa Tume wakati wa uchaguzi mkuu na kwamba Tume haipokei majina mapya.
“Bila ya kuathri masharti yaliyomo katika ibara hii, mtu yeyote atakuwa na sifa za kustahili kuchaguliwa au kuteuliwa kuwa Mbunge endapo; ni raia wa Jamhuri ya Muungano aliyetimiza umri wa miaka ishirini na moja, na ambaye anajua kusoma na kuandika katika Kiswahili au Kiingereza; ni mwanachama na ni mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa,” inasomeka sehemu ya Ibara ya 67 (1) ya Katiba.
Kailima anafafanua zaidi: “Baada ya kukamilisha utaratibu wa kupitia na kujiridhisha juu ya vigezo vya jina la mwanachama anayependekezwa, tunamwandikia Spika wa Bunge kumfahamisha kwamba tumeshafanya uteuzi, barua pia inatumwa kwa chama cha siasa kwa kunukuu barua yao ya maombi kuwafahamisha kwamba maombi yao yamepokelewa na yameshughulikiwa na wakati mwingine huwa tunawaandikia wahusika wenyewe (wabunge walioteuliwa).”
Akizungumzia suala mahususi la CUF, Mkurugenzi huyo wa Uchaguzi anasisitiza kwamba taratibu zilifuatwa. Kwamba Julai 26 Tume ilipokea barua kutoka kwa Spika kumfahamisha Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi kwamba kuna viti maalumu viko wazi Bungeni vya CUF.
Anasema siku iliyofuatia, Julai 27 Tume ilimwandikia katibu mkuu wa CUF. Kwa taratibu za tume, barua ikiandikwa na mwenyekiti wa tume inatumwa kwa mwenyekiti wa chama cha siasa na nikiiandika mimi (Mkurugenzi wa Uchaguzi) naituma kwa katibu mkuu wa chama husika”.
Anasema wakati wa kutuma barua, NEC imekuwa ikitumia anuani zilizotolewa na Msajili wa Vyama vya Siasa kwa sababu Tume haishughuliki na mambo ya usajili wa vyama na badala yake inapokea taarifa zote kuhusu majina ya vyama, majina ya viongozi, namba za usajili na anuani kutoka kwa Msajili.
Hata hivyo, Mkurugenzi huyo anakiri kwamba kuna vyama vina anuani zaidi ya moja kama CCM ambacho kina anuani ya Dodoma na Dar es Salaam na CUF ambacho kina anuani ya Dar es Salaam na Zanzibar.
Kailima anasema kwamba katika suala la CUF la hivi karibuni lililohusisha wabunge wanane waliotenguliwa na hatimaye Tume kuteua wabunge wengine, utaratibu ulifuatwa na barua kwa chama ilitumwa kwa anuani ya Dar es Salaam kwa kuwa barua iliyotumwa Tume ilitoka Dar es Salaam.
Akifafanua zaidi juu ya madai kwamba majina ya wabunge walioteuliwa hayakuwa kwenye orodha iliyotumwa awali na CUF, Kailima anasema matamshi au tuhuma kama hizo ni mfano tosha kabisa kwamba kuna watu, hasa wanasiasa ambao walijipanga kupotosha umma kwa makusudi kabisa kwa sababu za kisiasa wanazozijua wenyewe.
“Inashangaza kwa sababu Katibu Mkuu wa CUF, Seif Sharif Hamad ambaye anadai kwamba majina ya wateule hayakuwa kwenye orodha, yeye ndiye aliyesaini karatasi yenye orodha hiyo ambayo iliwasilishwa hapa Tume mwaka 2015,” anasema.
Akifafanua juu ya madai kwamba ni kwa nini tume ililishughulikia suala la CUF kwa haraka, Kailima anasema kwamba sheria ambazo zinaisimamia Tume kwenye mchakato wa uteuzi wa wabunge wa viti maalumu hazijaweka masharti ya muda kwenye uteuzi na kwa hiyo Tume ipo huru kufanya maamuzi haraka kadri iwezekanavyo na ni jambo linalopaswa kupongezwa na siyo vinginevyo. Mwandishi wa makala haya ni Afi sa Habari wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC.


Kumbukizi ya Nyerere vita ya Kagera yatia fora tamasha




Kama ulidhani Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere amesahaulika baada ya kifo chake mwaka 1999, basi umekosea.
Mawazo yake, vitendo vyake na dhamira zake bado zinaishi. Hayo yalijitokeza juzi kwenye tamasha la 36 la sanaa la kimatafa la Bagamoyo mjini hapa wakati kikundi cha maigizo cha Irene Sanga na produzya Mrisho Mpoto kilipofanya shoo.
Pamoja na usiku kuwa mwingi, saa tano, bado watazamaji wa igizo hilo maarufu kwa jina la Juliana lilionekana kusubiriwa kwa shauku na watazamaji wengi, wakubwa kwa watoto.
Hii ilitokana na kuwa igizo lililosheheni watu wenye vipaji vya uigizaji kama Oscar Nyerere anayesifika kwa kumwigiza Hayati Mwalimu Nyerere kwa sauti, vitendo, mavazi na hata mwonekano wa nywele zake zenye mvi nyeupe.
Zaidi linavutia kutokana na kuwa na msanii mwenye sauti na mbwembwe za kughani na kuimba kama Mrisho Mpoto halisi tofauti na zao zikiwa ni maumbile ya mwili na rangi. Lakini pia linavutia kutokana na kuwa na washiriki wenye haiba ya Rais wa zamani wa Uganda, Idd Amin Dada au Nduli nafasi ambayo imechezwa na mtu aliyeshiba vizuri na mrefu, mweusi kama Amin halisi huku kichekesho kikiwa cha Mkuu wa Majeshi wa zamani Tanzania, Jenerali David Musuguri kuwa dada mfupi, machachari na mkakamavu, Igizo hilo lilikuwa likirejerea historia ya vita ya Uganda ya mwaka 1978/79 ambapoTanzania ilimpiga Nduli hadi akakimbia uhamishoni huko Arabuni alikofia akiiacha nchi ikianza kipindi kigumu cha wananchi kufunga mikanda kwa miezi 18 iliyotangazwa na Rais Nyerere kukabili mtikisiko wa uchumi uliotokea.
Igizo linawaonyesha wananchi wa Kagera wakilalamikia kuvamiwa na wanajeshi wa Uganda kabla ya Mwalimu Nyerere kutangaza vita akisema sababu ya kumpiga Amin tulikuwa nayo, uwezo wa kumpiga tulikuwa nao na nia ya kumpiga tulikuwa nayo akiitaka Juuiya ya kimataifa ielewe Amin ndiye alituchokoza.
Igizo hilo liliwaacha watazamaji wakivunja mbavu kucheka pale Mkuu wa Majeshi, Jenerali Musuguri alipokuwa akiliweka sawa jeshi lake kumsikiliza Amii Jeshi Mkuu, Rais Nyerere ambapo mtangazaji alimtambulisha dada mfupi, mkamavu, mwenye kishindo ndiye Musuguri.
Kwa wanaomfahamu Musuguri halisi alivyo mtu wa miraba minne hawakuwa na namna zaidi ya kucheka na kufurahia ubunifu huo uliojaziwa na kishindo cha dada kuonesha ukakamavu uliostahili kuongoza kikosi kile.
Ni igizo lilolenga kuwakumbusha Watanzania kukabili matatizo ya kiuchumi kwa dhati pale yanapotokea matatizo badala ya kutafuta njia za mkato za kufanya biashara za magendo kama ambavyo baadhi waliamua kufanya magendo mpakani mwa Tanzania na Uganda, Mtukula.
Kabla ya igizo hilo, kundi la muziki wa asilia la Kunoga chini ya gwiji Saraganda lilitia fora kwa nyimbo sita likiacha watazamaji wakishangilia. Awali kulikuwa na kundi la Chivane band la Bagamoyo, JUNIOR sarakasi la Bagamoyo, mwera group, CD 4 na Revolution yaliyotamba huku Mrisho Mpoto na Malaika wakipanda pia na kusalimia kwa kughani na kuimba kidogo. Kwa hakika tamasha hili limesheheni uhondo.

Tuesday, 3 October 2017

Rais awataka madiwani Wanaotaka Kuongezewa Posho Wajiuzulu

Rais awataka madiwani Wanaotaka Kuongezewa Posho Wajiuzulu

SeeBait
Ongeza kichwa
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, amewataka madiwani wasio na shughuli ya kuwaingizia pesa binafsi kujiuzulu, kwani serikali yake haiwezi kuwaongezea posho wanayohitaji.

Akizungumza kwenye uzinduzi wa mkutano wa 33 wa Jumuiya Ya Tawala za Mitaa (ALAT) uliofanyika katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere Dar es salaam, amesema kwamba Madiwani hao walifahamu masharti ya kugombea nafasi hiyo, hivyo kama wameshindwa kuyatimiza ni vyema wakajiuzulu.

“Ndio maana diwani masharti tunapojaza fomu tunaambiwa lazima uwe na kazi maalum inayokupa kipato, sasa kama wapo madiwani waliojaza hiyo nafasi na hawana kazi ya kuwapa kipato, wajiuzulu udiwani”, amesema Rais Magufuli.

Leo katika hotuba iliyowasilishwa kwa Rais Magufuli ikisomwa na Mwenyekiti wa Jumuiya Ya Tawala za Mitaa (ALAT) Bwana Gulam Mkadam, waliomba kuongezewa posho za madiwani, kutoka Tsh. 300,000 hadi Tsh. 800,000 jambo ambalo Rais amelipinga.

Saturday, 23 September 2017

Iran yafanyia majaribio kombora lake

Iran yafanyia majaribio kombora lake

  • 23 Septemba 2017


Image captionIran inasema kuwa imefanyia majaribio kombora la Khorram-shahr.

Iran inasema kuwa imefanyia majaribio kombora la Khorram-shahr.
Kombora hilo lilionyeshwa hadharani katika maonyesha ya kijeshi jana Ijumaa.
Iran imesema kuwa kombora hilo linaweza kusafiri mwendo wa kilomita 2,000.
Kituo cha runinga cha taifa hilo kilionyesha picha za sherehe hizo.
Kombora la kwanza la Khorram-Shahr lilirushwa angani Januari lakini likalipuka katikati ya mwendo.



Image captionRais Donald Trump na rais Rouhani wa Iran

Jaribio hilo lilifanywa siku chache baada ya Rais Trump wa Marekani kushambulia Iran katika hotuba yake katika Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.
Rais wa Iran, Hassan Rouhani, ametetea hatua ya taifa lake kuimarisha zana zake kwa lengo la kujitetea.

Tuesday, 12 September 2017

Chadema yawashukuru wote waliomchangia Lissu


CAHAMA Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimewashukuru watu wote ambao wametoa michango yao kusaidia matibabu ya Tundu Lissu ambapo mpaka sasa zimepatikana Sh milioni 19.4. Kimesema hali ya mwanasheria wake huyo ambaye pia ni mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu inaendelea kuimarika taratibu.
Akielezea hali yake kwa masikitiko leo, Katibu Mkuu wa Chadema, Vicent Mashinji amesema hali yake juzi mchana ilikuwa mbaya ambapo ililazimu kumsaidia kupumua kwa kutumia mashine lakini baadaye hali yake iliimarika.
"Hiyo ndio hali ya Lissu, jana hali ikua mbaya ikabidi awekewe mashine ya kupumulia lakini mchana hali ikaimarika wakatoa mashine na asubuhi leo ameamka vizuri anaendelea kupigania pumzi yake," amesema Mashinji.
Mashinji amesema jana saa nne asubuhi alianza kupata matatizo ya kifua ambayo pengine yalitokana na kulala muda mrefu. Mashinji amesema mpaka jana ambayo ni siku ya tano tayari Lissu ameshafanyiwa zaidi ya upasuaji tatu na kwamba imebidi kusitisha upasuaji ili mwili upumzike.
Amesema kwa sasa matibabu yanayoendelea kwa Lissu ni sehemu za ndani ya mwili ambazo zingehatarisha afya yake na kwamba sasa wataanza kushughulikia viungo vya nje. Chama hicho kimewashukuru watu wote ambao wametoa michango yao kusaidia matibabu ya Lissu ambapo mpaka sasa zimepatikana Sh milioni 19.4.



Watu nane wanasadikiwa kuvamia na kuvunja jengo la Prime House lililopo mtaa wa Tambaza eneo la Upanga karibu na ofisi za Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) usiku wabkuamkia leo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Salum Hamduni amrthibitisha kuvamiwa na kuvunjwa kwa jengo hilo lenye ofisi mbalimbali ikiwamo ofisi ya Mawakili wa Prime Lawyers. Akizungumzia tukio hilo mmoja wa mawakili wa Prime Lawyers amedai kwamba mlinzi wa jengo hilo amekutwa amefungwa kamba miguuni na mikononi pamoja na mdomo kwa kutumia plasta.
"Kwa sasa ni mapema sana kujua ofisi gani zilizoathirika kwenye uvamizi uliotokea, polisi wanaendelea na uchunguz kujua nini kilichotokea," ameeleza wakili huyo. Akizunhumza kwa njia ya simu asubuhi, Kamanda Hamduni amesema Polisibwako eneo la tukio kwa uchunguzi wa awali ili kujua ofisi zilizoathirika kutokana na tukio hilona kusudio la wavamizi hao.

Watoto bado wanafanya kazi migodini, shambani’

Watoto bado wanafanya kazi migodini, shambani’   0 By Elizabeth Edward, Mwananchi eedward@mwananchi.co.tz Da...